
Ballotelli aliifungia Italia magoli mawili na kuifikisha nchi yake katika fainali ya Euro 2012
 
 
Mario Balotelli alifunga magoli 
mawili ya kupendeza mno na kuiwezesha timu yake ya Italia kuishangaza 
Ujerumani kwa kuifunga magoli 2-1 katika nusu fainali ya Euro 2012, na 
nafasi ya kucheza mechi ya fainali mjini Kiev dhidi ya Uhispania.
Mabao ya mshambulizi huyo wa klabu ya Manchester
 City ya England, aliingiza goli la kwanza wavuni kupitia kichwa, na 
pili kwa mkwaju wa kasi mno katika uwanja wa mjini Warsaw, na Italia 
kuwathibitishia Wajerumani katika kipindi cha kwanza kwamba ilikuwa na 
nia kamili ya kufika fainali. 
Wajerumani,
 kufuatia mshituko, walianza kucheza kwa makini zaidi, lakini bao lao la
 penalti, ambalo lilipatikana katika dakika ya 92, kupitia Mesut Ozil, 
lilichelewa mno, na halikuweza kuwaokoa.
Italia kamwe hawajawahi kushindwa na Ujerumani 
katika mashindano makubwa, na wamefanikiwa sasa kucheza mechi nane dhidi
 ya Ujerumani pasipo kushindwa. 
Hii sasa itakuwa mara ya tatu kwa Italia kuingia
 fainali za michuano hii ya mataifa ya Ulaya, na wataingia fainali kama 
timu inayodhaniwa kuwa dhaifu ikilinganishwa na mabingwa watetezi 
Uhispania. 
Timu hii ya meneja Cesare Prandelli ilistahili 
ushindi, kwani sio tu waliweza kupambana na Ujerumani ambayo iliwashinda
 wapinzani wao kwa urahisi, bali pia walifunga mabao yao mapema katika 
kipindi cha kwanza.
Timu hiyo ya Azzurri ilikuwa na nafasi 
ya kujiongezea magoli, lakini ilicheza kwa tahadhari kwa kuhofia kwamba 
iwapo ingeliongoza mashambulizi zaidi dhidi ya Italia, kulikuwa na 
uwezekano wa ngome yao kuachwa ikiwa dhaifu, na Wajerumani 
kuwashambulia.