BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Thursday, June 28, 2012

Mwanariadha wa Kenya matatani

Ezekiel Kemboi
Polisi nchini Kenya wamemchukulia hatua mwanariadha mashuhuri Ezekiel Kemboi kwa madai ya kumdunga kisu mwanamke mmoja Jumatano usiku.
Kemboi anasifika kwa mbio za mita elfu tatu kuruka viunzi na maji. Mwanamke anayedai kufanyiwa kitendo hicho, Anne Njeri Otieno, anadai kuwa mwanariadha huyo alimshambulia wakati alipokataa kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye.
Kemboi, aliambia polisi kuwa wakati alipokuwa anamrejesgha nyumbani mwanamke huyo katika mji wa Eldoret, walishambuliwa na watu wlaiokuwa wamejihami na hivyo akajeruhiwa kwenye purukushani hilo.
Kemboi mwenyewe ni afisaa wa polisi na anajiandaa kwenda mjini London kwa michezo ya Olimpiki.
Hata hivyo Kemboi aliachiliwa kwa dhamana baada ya kulipa dola 595 za Kimarekani na kesi yake itasikilizwa tena mwezi Septemba baada ya michezo ya Olimpiki.
"Tayari niko katika kikosi cha wanariadha watakaowakilisha Kenya kwenye michezo ya Olimpiki. Ninaomba mahakama kunipa nafasi niweze kushiriki " alinukuliwa akisema Kemboi mbele ya mahakama.
Mwandishi wa BBC mjini Eldoret Wanyama Chebusiri anasema kuwa Kemboi alichukua muda wa saa saba katika kituo cha polisi alipokuwa anahojiwa.
Kituo hicho cha polisi pia kilijaa watu waliokuwa wanataka kumuona Kemboi alipofika kwa mashtaka.
Hapo awali, Bi Otieno, ambaye anaendelea kupata nafuu hospitalini, aliambia waandishi wa habari kwamba alikuwa kwenye mkahawa mmoja na Kemboi wakati alipokubali kumpeleka nyumbani usiku ulipoingia.
Mwaka 2004 Kemboi aliyeshinda dhahabu kwenye mbio za elfu tatu aliambia polisi kuwa alivamiwa na wezi alipokuwa nje ya gari lake na kumtaka awape pesa na kisha kumshambulia.
Alisema alichukua hatua hiyo ili kujilinda dhidi ya kuvamiwa na katika purukushani hiyo Bi Otieno akajeruhiwa.

No comments:

Post a Comment

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...