MTU na mkewe waliokuwa wamelala eneo la Epsom, Surrey, Uingereza,
walishituka vibaya baada ya gari moja dogo ‘kuruka juu mita 24 (futi80)’
na kutua katika chumba walichokuwa wamelala.
Hii ilitokea majuzi wakati gari lenye rangi ya fedha aina ya Lexus lilipoigonga nyumba hiyo na kuharibu sehemu kubwa ya chumba hicho cha kulala ambapo polisi walisema kabla yake liliparamia gari aina ya Audi lililokuwa limeegeshwa.
Bahati nzuri, hakuna mtu aliyejeruhiwa katika tukio hilo lililotokea Barabara ya Bridge Road, wakiwemo watoto wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili.
Hii ilitokea majuzi wakati gari lenye rangi ya fedha aina ya Lexus lilipoigonga nyumba hiyo na kuharibu sehemu kubwa ya chumba hicho cha kulala ambapo polisi walisema kabla yake liliparamia gari aina ya Audi lililokuwa limeegeshwa.
Bahati nzuri, hakuna mtu aliyejeruhiwa katika tukio hilo lililotokea Barabara ya Bridge Road, wakiwemo watoto wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili.
No comments:
Post a Comment