Serikali ya Tanzania imetangaza
 kulifungia gazeti la MWANAHALISI kwa muda usiojulikana kutokana na 
kuandika habari na makala za uchochezi, uhasama na uzushi likiwa na nia 
ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya dola.
Taarifa iliyotumwa kwenye 
vyombo vya habari na ofisi ya msajili wa Magazeti Wizara ya habari, 
Vijana, Utamaduni na michezo imesema katika matoleo ya hivi karibuni, 
gazeti hilo limekua likichapicha habari na makala zenye kueneza na 
kujenga hofu kwa wananchi.
Taarifa imesema kabla ya uamuzi
 wa kulifungia Mwanahalisi, mhariri wa gazeti hilo aliitwa na kuonywa 
mara nyingi lakini hakuwa tayari kukiri kuwa maudhui ya makala zake 
hayakua na tija kwa jamii na zilikua hazifati madili ya uandishi wa 
habari japo amekua akinukuu kifungu cha 18 cha katiba ya Uhuru wa kutoa 
maoni ambapo hii ni mara ya pili kufungiwa, kabla liliwahi kufungiwa kwa
 miezi mitatu.
Unaweza kulike au kutweet hii post ili na wenzako waione.

No comments:
Post a Comment