SIKIA ALICHOSEMA WASTARA KUHUSU MUMEWE SAJUKI
Maombi ya watanzania pamoja na
michango yao ya fedha vimesaidia kumfikisha mwigizaji Sajuki hapa alipo
baada ya kupata nafuu kubwa toka apelekwe India kuitibiwa.
Wastara akizungumza exclusive
na millardayo.com amesema Sajuki anaweza kuanza kuigiza hata sasa kwa
sababu nguvu imesharudi, anaweza kutembea kwa muda mrefu na hata hali
yake ya sasa imebadilika sana tofauti na mwanzo.
Amesema “baada ya miezi mitatu
Sajuki anaweza kuanza kuigiza kama yeye mwenyewe atapenda na hata sasa
hivi alipo pale unaweza kwenda nae location hana wasiwasi wowote ila kwa
sababu ni mtu amefanyiwa upasuaji anahitaji kupumzika zaidi huwezi
kutoka nae kwa sababu kuigiza inahitaji akili zaidi lakini baada ya
miezi mitatu anaweza kuendelea na kazi”
kwenye sentensi nyingine
Wastara amesema hawezi kuzuia Sajuki kupigwa picha za Tv na magazeti kwa
sababu kupitia vyombo hivyo vya habari ndio walifahamu kwamba anaumwa
na wakaamua kumchangia sasa ni lazima wajue pia anaendeleaje kupitia
vyombo hivyo hivyo na sio kwamba anamdhalilisha.
No comments:
Post a Comment