HII INAWAHUSU MASHABIKI WOTE WA MAREHEMU KANUMBA.
Bado mpaka sasa kumbukumbu za
watanzania hazijalala, movie star marehemu Steven Kanumba bado
anakumbukwa kwa sababu bado kazi zake nyingi alizozifanya zinaendelea
kuonekana katika maisha ya kila siku ya watanzania wengi.
Wakati huu ambapo maonyesho ya
sabasaba yanakaribia kuanza Dar es salaam familia yake imeamua kuchukua
banda maalum kwenye viwanja vya saba saba kwa ajili tu ya kuendelea
kumuenzi Marehemu Kanumba.
Seth ambae ni Mdogo wake
waliekua wakiishi pamoja Sinza Dar es salaam amesema ni banda la Kanumba
litakalokua na Nguo zenye alama alizokua anazitumia Kanumba ikiwa ni
pamoja na jina na ujumbe, kutakua na picha zilizo kwenye frame za
Kanumba zinazomuonyesha toka akiwa utotoni, pia vikombe, kanga, bazee na
vitu vingine vingi vyenye alama na picha za Kanumba.
Seth amesema Mama mzazi wa
Kanumba pamoja na watu aliokua akifanya nao kazi Kanumba watakuwepo
kutoa maelezo mbalimbali kuhusu Kanumba na kazi zake.
No comments:
Post a Comment