BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Thursday, June 28, 2012

BOB JUNIOR aka CHOCOLATE FLAVOUR KUFUNGA NDOA JULY 1, 2012...!!!

  jestina george akipose na Bob Junior mwanzoni mwa mwaka huu alipokwenda UK kupiga kazi.
---
Mwanamuziki na producer anayemiliki studio ya Sharobaro Records, Bob Junior aka Mr. Chocolate Flavour, ameamua kufungua ndoa kwa style ya aina yake.

Amesema harusi yake itakayofanyika Jumapili ya tarehe moja mwezi July mwaka huu, pamoja na kufanyika nyumbani itatinga ndani ya club ya Billicanas ambapo kila mtu anaruhusiwa kuhudhuria.

Rais huyo wa masharobaro amesema wiki hii atapanda boti hadi Zanzibar kwenda kumfuata ‘mwali’ ili aisaliti rasmi kambi maarufu ya makapela.Bob Junior anayesifika kwa kukata ‘mauno’ kwenye video zake, amesema amechoka kuishi maisha ya ujana na sasa anahitaji kuwa na familia.

“Tunapiga show kila siku na kupata hela nyingi kwanini nisioe,” aliiambia 255 ya Clouds Fm jana.

Aliongeza kuwa dhumuni la kuamua kuoa ni kuepukana na vishawishi na maradhi kwakuwa watu maarufu kama yeye hujikuta wakitafutwa sana na wasichana.
Kila lakheri Bob Junior.

No comments:

Post a Comment

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...