Kwa longtime sasa hivi Tanzania
imeshuhudia magazeti mengi pamoja na stori za internet kwenye blogs,
website na facebook kuhusu Freemasons, kwa kiasi kikubwa baada ya hizo
habari, picha iliyojengeka kuhusu Freemasons ni kwamba ni dini ya
kishetani.
Wametajwa mastaa mbalimbali wa
Tanzania pamoja na viongozi wa kisiasa kwamba nao wamejiunga na dini
hiyo akiwemo rais mstaafu wa Tanzania William Mkapa na Rais Mwai Kibaki
wa Kenya.
Exclusive kwenye THE INTERVIEW
ya CLOUDS TV Mtangazaji Gerald Hando amefanya interview na Sir Andy
Chande ambae alikua freemasons lakini kwa sasa amestaafu.
Moja kati ya mambo
aliyoyazungumzia ni pamoja na taarifa za Kibaki na Mkapa kuwemo kwenye
hicho chama, hapa namkariri akisema “Hakuna hata mmoja kati ya mkapa
wala kibaki ambae ni Freemason, nilipofika hapa mwaka 1950 katika
biashara zangu nilikutana na watu wengi katika Nyanja mbalimbali ambao
walikuwa wakiandaa chama cha freemasons ambao walinialika kwenye vikao
mbalimbali Uganda, Kenya, uingereza na kwingineko kama Ghana na Khumasi
ila nikastafu baada ya miaka 19 kufanya kazi na freemasons.
Sihusiki tena na freemasons
huku Tanzania, ila kama uingereza naenda mara kwa mara kwa sababu bado
kuna baadhi ya mashirika ninayofanyakazi nayo hadi sasa, Freemasons sio
kama watu wengi wanavyosikia au kuambiwa.. kuna tofauti”
Baadae hapahapa millardayo.com
nitakuletea interview kamili kuhusu mengine aliyosema kuhusu maana ya
Freemasons, kazi zao na mengine.
No comments:
Post a Comment