BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Thursday, August 2, 2012

HII NDIO PICHA YA KWANZA KUMUONA SNOOP DOGG BAADA YA KUTANGAZA KUIMBA REGGAE!


.
Inawezekana ni njia mpya ya kutaka kuteka watu na kutengeneza hela kwa aina mpya ya biashara baada ya kukaa kwenye muziki kwa miaka ishirini, huu ni uamuzi wa rapper Snoop Dogg ambae sasa amebadilisha jina na kujiita Snoop Lion ameutangaza.
Ametangaza kuanza kuimba muziki wa Reggae anaouita muziki wa upendo, muziki atakao kuwa huru kuuperform hata kwa bibi, babu na watoto kwa sababu una mapokezi kwa marika yote tofauti na muziki wake wa kigumu alioufanya kabla.
Snoop Lion amesema alichofahamu kutoka kwa Marasta ni kwamba sio dini kama watu wanavyofikiria pia kuhusu jinsi wanavyoishi, amegundua kitu kingine tofauti pamoja na kusisitiza kwamba amekua rasta kwa kipindi kirefu lakini alikua hajafungua jicho la tatu ili kuligundua hilo, ila baada ya kufungua ndio amefahamu.
Kubadili jina na kuanza kufanya muziki wa Reggae hakua amekupanga, anasema ni hisia zilikuja tu na akaamua kuzifata, baada ya hapo ndio akasafiri mkapa Jamaica na kuingia kwenye studio ambayo aliiagiza imtengenezee kazi za ukweli za Reggae ambazo alizifurahia na kuzifanyia kazi.
Snoop mwenye umri wa miaka 40 ambae kipimo cha DNA kilionyesha kwamba asili yake sio Asia bali ni Africa 75%, 23% Native American na 6% European amesema haimaanishi kwamba muziki wa rap aliokua akiufanya mwanzo ni mbaya na kwamba anauacha bali anafanya muziki ulio kwenye hisia zake kwa sasa ambao ni reggae.

No comments:

Post a Comment

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...