BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Tuesday, July 10, 2012

SIMU ANAYOUZA JOSE CHAMELEONE WA UGANDA, ZIJUE BIASHARA ZAKE NYINGINE.

Millard Ayo na Jose Chameleone kwenye interview.
Kwa mara ya kwanza toka Show ya AMPLIFAYA ianzishwe zaidi ya siku 500 zilizopita, leo ndio interview ya kwanza na staa wa Afrika Mashariki Jose Chemeleone kutoka area 256 imesikika akiwa na Millard Ayo. Utazisikia Stori zake nyingi tu kwenye mfululizo wa show za AMPLIFAYA on super brand Clouds fm na hapa millardayo.com!!! kuhusu muziki wake najua hizo stori utakua umezisikia sana kwengine…. Ninachokifanya ni kwenda deep zaidi kwenye maisha yake, Navifata vyote vilivyotokana na jina lake. Huu ni mwaka wake wa 12 toka ameanza kuwa maarufu kwenye muziki, Jose Chameleone anaetajwa kuwa kwenye list ya wanamuziki watano matajiri wa muziki wa sasa Afrika Mashariki, leo amekubali macho yako yasome vitu atakavyovitaja vinavyompa pesa nyingi tofauti na muziki kwa sasa.
Hii ndio simu inaitwa CHEMELEONE ambayo inauzwa kwenye maduka mbalimbali Uganda, unaweza kuwaka line yoyote ya mtandao wa simu.

Amesema Moja kati ya ishu anazopiga ni “kununua nyumba na kuziuza, kukodisha, pia kununua mashamba na kuyauza huko Uganda, na kuna biashara nyingine nimeianza juzi juzi ya CHAMELEONE MOBILE, nilikwenda China na kuungana na kampuni moja ya China wakatengeneza simu inaitwa CHAMELEONE, hiyo ni moja kati ya kazi zangu kubwa… watu wanazinunua sana nyumbani Uganda, ni handset ambayo unaweza kuweka line ya mtandao wowote”
Kwenye line ya mwisho ChameleonE kasema “hii ni kujaribu kufikiria nje ya box pamoja na kujaribu kufanya mipango uliyokua nayo kichwani, na bado naendelea baada ya hizo simu nataka kutengeneza vitu vingi zaidi.. nataka jamii yangu inikumbuke kwa nilichowafanyia”
Hayo ndio aliyoyasema Staa wa muziki Jose Chameleone wa Uganda nchi inayotajwa kuwa na wasanii wanaoongoza kwa kuwa na pesa nyingi kuliko nchi yeyote Afrika Mashariki.
Tayari mpaka sasa kuna baadhi ya mastaa ambao wamejaribu kupiga dealz nyingine mbali na muziki akiwemo Lady JayDee ambae anamiliki Mgahawa, Jua Cali wa Kenya alitangaza kuanza kutengeneza headphone kama za Beat by Dre, Profesa Jay nae alitangaza kwamba ndoto zake hazipo kwenye magari ya kifahari sasa hivi au anasa nyingine, anajipanga kwa ajili ya kuinvest kwenye ardhi for now.

No comments:

Post a Comment

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...