Kama unakumbuka Siku 49 
zilizopita, Mwimbaji wa zamani wa Bongo fleva ambae sasa ni mwimbaji wa 
nyimbo za Injili Stara Thomas kupitia AMPLIFAYA alitaja sababu za yeye 
kushindwa kufanya kolabo na wasanii wengine wa gospel kwenye album yake 
mpya na ya kwanza toka aokoke mwaka mmoja uliopita.
Alisema “kwenye upande wa 
Injili waimbaji wengi bado hawajawa na ufahamu wa kufanya kolabo japo 
lile ni neno la Mungu linalosimama peke yake haijalishi mnashirikiana au
 hamshirikiani lakini kushirikiana ni jambo jema, ugumu ambao nimeuona 
na nimejifunza ni kuhusu unafiki mkubwa sana, mtu anaweza kukuchekea 
machoni lakini moyoni ni muongo, kuna wengine wasanii wakubwa niliwaona 
nikafikiri lakini nilipowakaribia nikagundua sio, unafiki ni mwingi, 
kule kwenye bongofleva kulikua kuna upendo”
.Baada ya hayo, Mchungaji 
mtarajiwa ambae pia kwa sasa ni mwimbaji wa nyimbo za injili pia, 
mchekeshaji Masanja Mkandamizaji wa Orijino Komedi amekubali kutoa wazo 
lake kuhusu ishu ya Stara kukosa ushirikiano wa kutosha kwa wasanii wa 
Gospel aliowategemea.
Hii ndio kauli yake….. “Hii 
kazi inayofanyika huku kwenye Gospel ni huduma sio biashara, hii ni 
huduma tunayoifanya kwa hiyo mwanadamu yeyote, wito kwa Stara na wasanii
 wengine wanaotoka kwenye bongofleva na kuja kwenye Gospel na kukutana 
na hivi vitu, ulichofata kwenye Gospel sio kolabo na flani, umefata 
kufanya huduma ya wewe na Mungu wako fanya hiyo kwa sababu hata 
usiposhirikia na na mtu bado kazi yako ikifanywa mbele za Mungu 
itahesabiwa haki, umeokoka ili umtumikie Mungu.. mtumikie uachane na 
binaadam kwa sababu sio wote wanaoimba Gospel wanamcha Mungu, kuna 
mwingine anaimba Gospel kama biashara sasa ukisema mshirikiane akakataa 
itakuumaje na wewe unamtumikia Mungu?”
Hii sio mara ya kwanza kwa 
wasanii waliotoka kwenye bongofleva mpaka kuokoka na kufanya muziki wa 
Gospel kutoa hayo malalamiko, mwigizaji Dokii pia alishawahi kuwachana 
sana na kusema wasanii watano wakubwa wa Gospel Tanzania hakuwataja kwa 
majina lakini alisema ndio wanafiki wakubwa, wana ubinafsi, chuki, 
kujisikia na kujitenga na hawakukubali kumpa ushirikiano wowote.
Waimbaji wa Gospel wenyewe 
wameshawahi kukiri kwamba hakuna upendo kati yao, watu wanachukiana, 
hawana umoja.. Rose Muhando, Upendo Nkone na Miriam Mauki walishalisema 
hilo kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM.

No comments:
Post a Comment