BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Wednesday, July 25, 2012

ALICHOSEMA MASANJA MKANDAMIZAJI KUHUSU MALALAMIKO YA STARA THOMAS KWENYE MUZIKI WA INJILI


Masanja Mkandamizaji akiwa kwenye shooting ya moja ya video zake za Gospel.
Kama unakumbuka Siku 49 zilizopita, Mwimbaji wa zamani wa Bongo fleva ambae sasa ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Stara Thomas kupitia AMPLIFAYA alitaja sababu za yeye kushindwa kufanya kolabo na wasanii wengine wa gospel kwenye album yake mpya na ya kwanza toka aokoke mwaka mmoja uliopita.
Alisema “kwenye upande wa Injili waimbaji wengi bado hawajawa na ufahamu wa kufanya kolabo japo lile ni neno la Mungu linalosimama peke yake haijalishi mnashirikiana au hamshirikiani lakini kushirikiana ni jambo jema, ugumu ambao nimeuona na nimejifunza ni kuhusu unafiki mkubwa sana, mtu anaweza kukuchekea machoni lakini moyoni ni muongo, kuna wengine wasanii wakubwa niliwaona nikafikiri lakini nilipowakaribia nikagundua sio, unafiki ni mwingi, kule kwenye bongofleva kulikua kuna upendo”
.Baada ya hayo, Mchungaji mtarajiwa ambae pia kwa sasa ni mwimbaji wa nyimbo za injili pia, mchekeshaji Masanja Mkandamizaji wa Orijino Komedi amekubali kutoa wazo lake kuhusu ishu ya Stara kukosa ushirikiano wa kutosha kwa wasanii wa Gospel aliowategemea.
Hii ndio kauli yake….. “Hii kazi inayofanyika huku kwenye Gospel ni huduma sio biashara, hii ni huduma tunayoifanya kwa hiyo mwanadamu yeyote, wito kwa Stara na wasanii wengine wanaotoka kwenye bongofleva na kuja kwenye Gospel na kukutana na hivi vitu, ulichofata kwenye Gospel sio kolabo na flani, umefata kufanya huduma ya wewe na Mungu wako fanya hiyo kwa sababu hata usiposhirikia na na mtu bado kazi yako ikifanywa mbele za Mungu itahesabiwa haki, umeokoka ili umtumikie Mungu.. mtumikie uachane na binaadam kwa sababu sio wote wanaoimba Gospel wanamcha Mungu, kuna mwingine anaimba Gospel kama biashara sasa ukisema mshirikiane akakataa itakuumaje na wewe unamtumikia Mungu?”
Hii sio mara ya kwanza kwa wasanii waliotoka kwenye bongofleva mpaka kuokoka na kufanya muziki wa Gospel kutoa hayo malalamiko, mwigizaji Dokii pia alishawahi kuwachana sana na kusema wasanii watano wakubwa wa Gospel Tanzania hakuwataja kwa majina lakini alisema ndio wanafiki wakubwa, wana ubinafsi, chuki, kujisikia na kujitenga na hawakukubali kumpa ushirikiano wowote.
Waimbaji wa Gospel wenyewe wameshawahi kukiri kwamba hakuna upendo kati yao, watu wanachukiana, hawana umoja.. Rose Muhando, Upendo Nkone na Miriam Mauki walishalisema hilo kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM.

No comments:

Post a Comment

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...