Mamia ya Mau Mau wamerundikwa kwenye kambi
Mashirika ya kupigania haki za 
kibinadamu zimeishutumu serikali ya Kenya kwa kukataa kugharimia kesi 
ambayo wapiganaji wa zamani wa Mau Mau wameishitaki serikali ya 
Uingereza.
Wapiganaji hao wazamani tayari wamewasili Mjini 
London kushitaki wakoloni walioitawala Kenya kwa madai ya kuwatesa 
wakati wakipigania uhuru wa Kenya.
Awali serikali ilitangaza kuwa inaunga mkono kesi hiyo ya Mau Mau.
Lakini wakuu wa serikali wameshindwa kueleza ni kwa sababu gani hawagharimii kesi hiyo.
George Morara alihoji kwanini serikali ya Kenya 
haitaki kuwasaidi Mau Mau ambao walipigania uhuru wa Kenya wakati 
serikali hiyo hiyo sasa inawasaidia wakenya mashuhuri ambao 
wameshitakiwa katika mahakama ya uhalifu wa kimataifa-ICC.
Mwanaharakati huyo amesema kuwa ingawa Mau Mau 
ilikuwa maarufu katika miaka ya 1950 hadi 60 lakini kuna baadhi ya 
viongozi wa serikali wanaohofia kuwa kesi hiyo huenda ikawadhuru 
kisiasa.
Mwandishi wa BBC wa Maswala ya Afrika Martin 
Plaut anasema imechukua muda mrefu kwa kesi hiyo kufikia hatua ya sasa 
na huenda ikachukuwa muda mwengine mrefu zaidi kwa Mau Mau kuthibitisha 
madai ya kuteswa na wakoloni wakati wakipigania uhuru wa Kenya.
No comments:
Post a Comment