BBB

advertisement

tangaza sherehe

ADVERTISEMENT

Wednesday, February 6, 2013

Beyonce Knowles and Jay-Z's Daughter Blue Ivy 'Starting to Talk'

Beyonce Knowles' daughter with Jay-Z is entering her 13 months old, and she is starting to talk. The proud mama reveals her little girl's major milestone when chatting on "Super Bowl Live" show ahead of her halftime performance in New Orleans. "She's starting to talk," Queen Bey opened up before gushing about motherhood, "[It's] the best thing in the world . . . It's just such a beautiful time in my life to have a child and every day see something new and see her learn something new." Beyonce, who miscarried two years ago, gave birth to baby Blue Ivy Carter on January 7, 2012. "My husband is incredible," she praised her hubby for being there for her in every journey through the ups and downs. "He's so supportive."

MANUMBA ALAZWA HOSPITALI ALIYOLAZWA MANDELA



Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, DCI Manumba alisafirishwa kutoka Hospitali ya Aga Khan jijini Dar siku kadhaa zilizopita kwa kutumia gari maalum la kubebea wagonjwa hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alikopakizwa kwenye ndege maalum ya Kampuni ya AAR kuelekea Bondeni baada ya afya yake kutengemaa kidogo.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Jaffer Dharsee, Manumba alisafirishwa baada ya kupata ahueni kidogo huku akiwa na uwezo wa kuchezesha viungo mbalimbali vya mwili wake, tofauti na hali aliyokuwa nayo awali.
Manumba alifikishwa hospitalini hapo Januari 13, mwaka huu baada ya kuhamishwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akiwa anasumbuliwa na malaria kali (vijidudu 500) vilivyosababisha figo zake mbili zipoteze uwezo wa kufanya kazi na kupoteza fahamu.

Hospitali ya Milpark jijini Johannesburg, Afrika Kusini alipolazwa DCI Manumba.
Uchunguzi uliofanywa na Risasi Mchanganyiko, umebaini kuwa hospitali aliyopelekwa kiongozi huyo wa jeshi, Milpark ina uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa ya dharura kama mshtuko wa moyo, mtikisiko wa ubongo, kiharusi, kupooza, kupandikiza figo na mapafu na matatizo mengine yanayohusu mfumo wa fahamu.
Hospitali hiyo yenye wodi 90 za wagonjwa mahututi, madaktari wazoefu na vifaa vya kisasa vya tiba, ikiwa na historia ya kuwatibu watu wengi mashuhuri barani Afrika, inatajwa kutoa huduma bora zaidi.
Miongoni mwa watu mashuhuri waliowahi kutibiwa hospitalini hapo, ni Rais wa Kwanza Mweusi wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ambaye alilazwa Januari 25, mwaka jana.

MATUMAINI AKWAMA KUTUA BONGO

INGAWA taratibu za kumrejesha nchini msanii wa vichekesho, Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ aliyeko Msumbuji kukamilika, amekwama Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maputo kutokana na kutokuwa na hati ya kusafiria.
Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’.
Matumaini yupo nchini humo ambapo inaelezwa kuwa ni mgonjwa na hali yake ni mbaya, hivyo ndugu zake kwa kushirikiana na wasanii kufanya taratibu za kumrejesha nchini.
Habari zinasema kwamba, taratibu za kumrudisha nchini zilikamilishwa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla ambaye alitoa tiketi lakini Matumaini alikwama kwa kukosa hati ya kusafiria.

Wakati ndugu na wasanii wakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar juzi Jumapili wakimsubiri ndipo taarifa zilipofika na kueleza kwamba amekwamishwa na hati ya kusafiria.
Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania, Michael Sangu ‘Mike’ ndiye aliyetoa taarifa hiyo akieleza amejulishwa na mtu aliyekuwa akishughulikia safari yake aliyeko jijini Maputo, Msumbiji.

Mike alisema: “Kila kitu kilikuwa tayari, tatizo ni mtu aliyepewa jukumu la kufuatilia pasipoti, hakuonekana airport, hivyo mtu anayehusika na vibali alikataa katakata kumruhusu kusafiri pamoja na kupewa maelezo mengi.”
Taarifa hiyo ilisababisha machozi kugubika miongoni mwa wasanii na ndugu wa msanii huyo, lakini juhudi zaidi za kufanikisha kurejeshwa nchini zinaendelea kufanyika.



BONGO MOVIES KUFANYA BONANZA




Wasanii wa sanaa za maigizo nchini ‘Bongo Movies’ wanatarajia kufanya bonanza litakalohusisha michezo mbalimbali kwa kushirikiana na wafanyakazi wa mahoteli ya kitalii jijini Dar es Salaam.
Akipiga stori na kona hii wikiendi iliyopita, Katibu Mkuu wa Chama cha Waigizaji Tanzania, Christian Kauzeni alisema kuwa lengo la tamasha hilo ni kuleta ushirikiano endelevu kati ya wasanii na wafanyakazi wa mahoteli.
Alisema: “Litafanyika Jumamosi ya Februari 9, mwaka huu katika Uwanja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama. Kutakuwa na michezo mbalimbali kama pete, mpira wa miguu  na michezo mingine mingi.”

PREZZO AND GOLDIE WEDDING SET FOR 9TH OF FEBRUARY!

LAST year on the 12 of November, reports about Prezzo being in Lagos to meet Goldie's parents for a traditional ceremony in which he officially asked for Goldie's hand in marriage rent the internets. Actually, i caught wind of the story from Big Brother Africa's site.
The ceremony i spoke of is known as “Ibankwu” by my Igbo people and I believe Kikuyus call it "Rurocio" or something close to that. According to Big Brother Africa's website, the wedding was set for the 9th of this month. Here's how they carried the article written by Joe:
"It is no longer news that Nigerian music queen Goldie and Kenya music president, Prezzo are an item. Goldie has always had a thing for men outside her home country Nigeria and even since when they were in the BBA house; they had been having a good relationship.
Though things went out of hands at the end of the show, their loves story continued after the show. Like a knight in shining armour, Prezzo headed for Nigeria to ask for his lovers hand in marriage. We can confirm that the two are set to marry. Last week in a formal ceremony at Goldie’s parents’ residence in Lagos, Nigeria, Prezzo asked for Goldie’s hand in marriage.
The wedding ceremony will hold in February 9th in Lagos. Prezzo promises to take the whole of Kenya down to Nigeria for the ceremony."

Tuesday, February 5, 2013

Not Exactly Breaking News: Britney Spears Sports Tacky Look







Britney's done it again!
The pop star, who's never had a chic street style, wore a particularly odd ensemble on Sunday, as she and her sons Sean Preston, 7, and Jayden, 6, took her pups to see the veterinarian in L.A. It was the kind of tacky, just-threw-on-whatever look that inspires people to jokingly write "y'all" every time they refer to her.
Spears donned pajama shorts, a tank top (with bra straps peeking out from underneath), tall patterned socks, sneakers, a messy updo, and what looks like makeup from the night before — an outfit that would have been perfectly accessorized with a bag of Cheetos.
Perhaps there was something seriously wrong with her adorable pooches, and she had to rush out of the house? Or, maybe she just wanted to give herself a break on a lazy Sunday?
Unfortunately, when you're Ms. Britney Spears, there are always cameras watching.
Whatever her reason for choosing the getup, it's a far fall from the more pulled-together mini dress looks she was sporting on "The X Factor" last season.




Now that she's parted ways with the reality competition, Brit Brit is focusing on making her own music.
Just last week, the "3" singer tweeted that she was back behind the mic.
"I'm at the studio recording a new song for my boys," she wrote. "They are going to freak out when they hear it. So excited! It's a surprise so keep it shhhhh and don't be grouchy. I'll fill you all in soon ;)"
Then again, who cares what she's wearing? We'll take some more of that music, please!















Justin Bieber and Selena Gomez Reunite in L.A… and N.Y.C.?


 




Justin Bieber and Selena Gomez are having a hard time walking away from each other.
Technically off-again after their split in early January, the exes spent time together over the weekend in L.A. ... and a New York City rendezvous could be next!

ASKARI POLISI ATELEKEZA MTOTO ITUONI

ASKARI moja aliyekuwa zamu katika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Wilaya  ya Temeke jijini Dar es Salaam ambaye jina lake halikupatikana mara moja alipigwa na butwaa baada ya kutelekezewa mtoto (pichani) na raia mmoja Januari 26, mwaka huu.
Vyanzo vyetu vya habari vilidai kwamba siku hiyo mwanaume mmoja alifika kituoni hapo akiwa na mwanaye wa kiume mwenye umri wa miezi minne na aliwaeleza askari kwamba mkewe amemtelekezea mtoto huyo kisha kwenda  kusikojulikana.
Taarifa zaidi zilieleza kwamba
 baada ya baba huyo kufika ‘kaunta’ na kumweleza polisi aliyekuwa zamu kwamba hana pa kumpeleka mtoto huyo, aliwaomba wabaki naye kituoni hapo hadi mkewe atakapopatikana.
Habari hizo zilieleza kwamba polisi huyo alimweleza baba wa mtoto kwamba ampeleke kwa ndugu zake ili wamlee, ambapo
alikubali na kuamua kumfunga mtoto mgongoni lakini askari alipotoka kidogo akapata nafasi ya kumtelekeza  mwanaye juu ya meza pale kituoni na kutoweka.
Habari zinasema askari  aliporudi alimkuta mtoto akitabasamu akiwa juu ya meza lakini baba yake hakuonekana  kwa muda mrefu, ndipo walipoamua kumpeleka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati wazazi wake wanatafutwa.
Mwandishi wa habari hii alipofika Muhimbili, Afisa Ustawi wa Jamii Jengo la Watoto, Virginia Mwabena alikiri kuwepo kwa mtoto huyo hospitalini hapo.
‘‘Tuliletewa mtoto huyo na askari PC Bilikuza mwenye namba 5862 wa Kituo cha Polisi Chang’ombe akidai mtoto alitelekezwa na baba yake kituoni,” alisema afisa huyo.
Hata hivyo, wananchi waliokuwepo hospitalini hapo walilaani kitendo hicho cha wazazi kumtelekeza mtoto huyo asiye na hatia ambaye bado anahitaji malezi ya baba na mama yake.

MFANYA BIASHARA AMPIGA MTU RISASI

MFANYABIASHARA wa mbao jijini Dar Salaam, Chacha Karongwe ‘Amang’ana’, wiki iliyopita alimpiga risasi kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Frank Filus, mkazi wa Tandika Mtaa wa Nasi B, kisa  kikitajwa ni  shilingi 100 inayodaiwa haikulipwa kwa ajili ya maji.
Frank Filus aliyepigwa risasi na mfanyabiashara wa mbao, Chacha Karongwe.
Majeruhi huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Temeke, wodi na 7 alipohojiwa na gazeti hili alisema chanzo cha hayo yote ni shilingi 100 ambayo mama yake aliambiwa hajailipa kwa mke wa mtu aliyempiga risasi kutokana na maji aliyochota kwake.
“Mama yangu anayeitwa Sara Mwakatale alikwenda kuchota maji saa 12 jioni na hapakuwa na mtu wa kupokea fedha na kaacha  shilingi mia moja pale bombani, mara nyingi ndivyo tunavyofanya.
“Baadaye mama mwenye maji alimtolea maneno mabaya mama na akamuita mumewe ambaye naye alifanya kama mkewe, hali iliyomshangaza mama ambaye alimuuliza kwa nini anaingilia mambo ya wanawake.
“Mama alinipigia simu akanieleza mkasa nikarudi nyumbani, maelezo yake yalinifanya nimfuate Chacha  ambaye aliniambia kuwa alikuwa ananitafuta siku nyingi ndipo aliingia ndani na kutoka na bastola.
“Alipiga risasi moja ikanikosa shingoni, ya pili ikapita hewani lakini ya tatu ikanipiga pajani na kunivunja na hadi hivi sasa risasi hiyo haijatolewa,” alidai Frank.
Gazeti hili lilikwenda eneo la tukio na kukutana na Mjumbe wa Shina namba 45, Tandika Kilimahewa,  Rajabu Zuberi ambaye alisema kuwa wakazi wa eneo hilo wamesikitishwa  na tukio hilo kwa sababu haijawahi tokea mtaani kwao, kwanza  ni tukio la aibu mtu kupigwa risasi kwa sababu ya shilingi 100.
Kwa upande wa mke wa anayedaiwa kupiga risasi, Felistiana Chacha alisema kuwa mama Frank alichota maji bila kulipia shilingi 100 na alipomtuma mtoto kudai mama huyo alirudi na kumtukana hivyo akaenda Kituo cha Polisi Tandika Kilimahewa alikofungua kesi yenye jalada namba CHA/RB/792/2013 Lugha ya matusi na mtuhumiwa akakamatwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englebert Kiondo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema upelelezi unaendelea.

UDAKUZZZ


KWA STORY ZAIDI NUNUA MAGAZETI YA GLOBEL PUBLISHERS!!!!

MTOTO WA AJABU AZALIWA IRINGA

“HUJAFA hujaumbika, Mungu ana makusudi yake na yeye  ni muweza  wa  yote kwani ndiye  aliyeumba mbingu na nchi na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.” Hiyo ni kauli ya mzazi wa mtoto  Zawadi Godfrey Mwingune aliyezaliwa akiwa na macho matatu na kichwa mfano wa uyoga.
.
Akizungumza na gazeti hili wiki iliyopita mama mzazi  wa mtoto  Zawadi, Marthar Kitago (28) mzaliwa wa  Kijiji cha Kidegembye Lupembe wilayani Njombe mkoani Njombe  alisema  kuwa hadi sasa anamwachia Mungu ambaye ndiye amempa zawadi ya mtoto  huyo.
“Jumapili Januari 13, mwaka huu nilishikwa na uchungu nikakimbizwa katika  Kituo cha Afya cha  Kidegembye ambako sikukaa nikahamishiwa Hospitali ya Wilaya ya Njombe  Kibena ambako nilifanyiwa upasuaji na kubahatika kumpata mtoto huyu.
“Niliogopa sana baada ya kuonyeshwa mtoto wangu
jinsi alivyo ila nilipiga moyo konde kwa kuwa ni damu yangu, tukampa jina la Zawadi, tukiwa na maana ni kutoka kwa Mungu,” alisema mama huyo wa watoto watatu.
Baba wa mtoto huyo, Godfrey Mwingune anayeendesha maisha yake kwa kilimo alisema kuwa hali ya afya ya mtoto huyo si nzuri kwani mbali ya kuzaliwa na kilo 4 na nusu, bado ana tatizo la uvimbe katika paji lake la uso unaofanana na umbo la uyoga pia  kichwani kuna kovu kubwa kama ncha mbili hivi ambalo linatoa usaha mwingi.
Akaongeza kuwa katika jicho lake la  kushoto kwa juu kuna jicho la pili na kufanya mtoto huyo kuwa na macho matatu ambapo madaktari  wamemshauri ampeleke katika  Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Amesema fedha zinazotakiwa ili mwanaye apatiwe tiba ni shilingi 1,500,000 na amewashukuru wakazi wa Isimani ambao  wamemchangia shilingi 300,000 kwani yeye hana uwezo.

Walioguswa na habari hii wanaweza kumchangia mtoto huyu kupitia namba 0754 026 299 au   
0712 750 199- Mhariri.

LULU AMTEMBELEA WASTARA


 


MWISHONI mwa wiki iliyopita, msanii Elizabeth Michael “Lulu” alikwenda kumpa pole msanii mwenzake Wastara Juma kwa kufiwa na mumewe, Sajuki...

Huzuni ilitawala nyumbani kwa Wastara mara baada ya Lulu kuwasili, lakini hatimaye baada ya muda mrefu wa maongezi nyuso za wasanii hao zikapambwa na tabasamu.

SHARE

TOA MAONI YAKO KUHUSU POST HII

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...